Monday, November 19, 2012

HAKUNA AJIRA MIJINI.

  • TAKRIBANI WALIMU WAPYA 28638 KUPELEKWA VIJIJINI.

Naibu Waziri wa Elimu Philip Mulugo(kushoto)
Serikali imetangaza mpango mpya wa ajira za walimu 28,638 wa Shule za Msingi na Sekondari katika mikoa minane. 
Mikoa hiyo ni ile ambayo inakabiliwa na changamoto ya uduni wa miundo mbinu, mazingira bora ya kufanyia kazi na kukosa motisha  kwa wafanyakazi kama vile nyumba za kuishi.
 
Utaratibu huo wa ajira mpya hautahusisha  majiji na manispaa ambako walimu wengi hukimbilia  baada ya kupata ajira na serikali imepanga kuwachukulia hatua watumishi wake zaidi 800 waliotoroka kazini na kujiunga na vyuo vya elimu ya juu bila idhini ya mwajiri.


Hatua hiyo ilitangazwa na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo, aliyoitoa wakati akizungumza na wahitimu zaidi ya 700 wa Chuo Kikuu cha Elimu Mkwawa (MUCE) kilichopo mkoani Iringa.
 
Mulugo alisema licha ya kuamua kuajiri walimu 28,638 idadi ya walimu wote waliohitimu kwenye vyuo vinavyotoa mafunzo hayo haikamilishi idadi hiyo.


 “Wote hapa, tutawaajiri, lakini safari hii, hakuna ajira mijini na wote mtakaoajiriwa, tunawapeleka katika wilaya zenye changamoto, kwa hiyo mtakwenda mikoa ya Katavi, Kigoma, Rukwa, Mbeya, Shinyanga, Manyara, Mtwara na Lindi. Tamko la serikali ndio hilo na mfahamu kabisa kwamba ajira hizi hazitahusu majiji na manispaa,” alisema Mulugo.


Alisema ajira hizo zitangazwa rasmi Januari mwaka 2013 huku akionya kuwa wahitimu hao wa shahada ya kwanza ya ualimu katika fani mbalimbali wasithubutu kuwashawishi maofisa waandamizi wa wizara kuomba kuteuliwa kuwa maofisa elimu wa wilaya na mikoa.
 
Kuhusu walimu waliotoroka kazini na kujiunga na vyuo vya elimu ya juu pasipo ridhaa ya mwajiri, Mulugo alisema serikali imegundua kuwa tatizo hilo limeiathiri zaidi mikoa iliyopo Kanda ya Ziwa na mikoa ya Kaskazini ambayo inakabiliwa na uhaba mkubwa wa walimu.


 “Nawatangazia kiama wale ambao walitoroka kazini na kuja kujiunga na vyuo vya elimu ya juu pasipo ridhaa ya mwajiri wake…Wizara imewaagiza maofisa elimu wa Wilaya na Mikoa kuleta haraka majina hayo wizarani ili tuchukue hatua kali,” alisema Mulugo.




SOURCE:
Nipashe
November 19,2012.

Friday, October 26, 2012

TAKRIBANI WAFANYAKAZI 78 MGODI WA RESOLUTE (T) LIMITED NZEGA WAPUNGUZWA KAZI.

                                  Katika kile kinachosemekana kuwa ni hatua za mwanzo za kufungwa kwa mgodi wa dhahabu wa Lusu uliopo katika kata ya Lusu wilayani Nzega mkoani Tabora unaomilikiwa na kampuni ya uchimbaji madini ya Resolute Goldmine (T) Limited,wafanyakazi takribani 78 wamepunguzwa kazi mwishoni mwa mwezi September.
Wakizungumzia sakata hilo,baadhi ya wafanyakazi hao wamesema zoezi hilo litakuwa endelevu na litafanyika kila mwisho wa mwezi ama wakati wowote endapo kampuni itaona inafaa kufanya hivyo.Aidha wafanyakazi hao wamesema kuwa Kampuni imechukua maamuzi hayo kutokana na kupungua kwa shughuli za uzalishaji katika kampuni hiyo."Shughuli za uzalishaji zimepungua sana kwa sasa,tena kuna mpango wa kupunguza wafanyakazi wengine tarehe 15 mwezi huu na sio mwisho wa mwezi tena".Alisema mmoja wa wafanyakazi wa kampuni hiyo aliyebahatika kuukwepa mchujo wa kwanza.
Aidha taarifa za ndani kutoka katika mgodi huo zinadokeza kuwa mpaka kufikia mwishoni mwa mwaka huu kampuni ya Casspian ambayo inafanya shughuli za uchimbaji katika mgodi huo haitakuwa na chake tena.
"Mali haijaisha,tena bado ipo nyingi sana ila nahisi mkataba ndo umekwisha au kuna issue nyingine inaendelea na kuna uwezekano kampuni nyingine ikaja kutake over".Alisema pia mmoja wa wafanyakazi aliyenusurika katika mchujo huo wa kwanza.


Itaendelea..............

KUKITHIRI KWA AJALI ZA KUTISHA TANZANIA,NINI KIFANYIKE?

 Wimbi la ajali TANZANIA lazidi sababisha vifo na majonzi mioyoni mwa Watanzania lukuki.

                        

   Basi la Kampuni ya Dar Express likiungua na kuteketea kwa moto katika barabara ya Segera –Chalinze eneo la Kijiji cha Segera, mkoani Tanga.               

            


                          
Baadhi ya wananchi wakishangaa mabaki ya moja ya magari ambayo yaliwaka moto uliotokana na Lori la mafuta kulipuka na kuwaka moto.Katika ajali hiyo ya kusikitisha,watu kumi walikufa papo hapo, huku mbunge wa viti maalum Dk Mary Mwanjelwa akijeruhiwa.

JE UNADHANI NINI KIFANYIKE?.

HAKUNA LISILOWEZEKANA.

                          



Hakika Mungu si mchoyo na hivyo hawezi kukunyima kila kitu.Wakati wanaharakati wa haki za binadamu kila pande Duniani wakiendelea kulalamikia miundombinu isiyo rafiki kwa walemavu,mlemavu huyu alionekana akiendesha baiskeli ya miguu miwili kando kando ya Barabara ya Msasani, jijini Dar es Salaam,hivi karibuni.
Hii inatafsiriwa kama ujumbe kwa walemavu wote kwamba hakuna lisilowezekana endapo watathubutu kwani kwa hali ya kawaida ni kama ndoto au jambo lisilowezekana kumuona mlemavu kama huyu akiendesha baiskeli yenye magurudumu mawili.Hii ni kutokana na ukweli bayana kwamba wengi wetu tumezoea kuwaona walemavu wakiendesha baiskeli zenye miguu mitatu ama minne.